Tuesday, July 27, 2010

10 Things You Didn't Know About Kim Kardashian




10 ) Kim was nominated in 2009 for the Razzie Award for Worst Supporting Actress for her
performance in Disaster Movie.

9 ) She has had sex on an airplane.
"On a private plane though. I don’t think I’d do it on a commercial flight."

8 ) "She lost her virginity to R. Kelly's soundtrack."

7 ) She hates dirty feet in bed and washes them before hitting the sheets.


6 ) In 2009, Kim had a severe case of sunburn she got on a trip to Mexico that made the news.

5 ) She used to be a celebrity closet organizer.

"The hardest celebrity closet to organize was Paris Hilton's because she had so many clothes that she had to convert a bedroom into a close.

4 ) Her first boyfriend was Tito Jackson’s son. Kim's family were friends with the Jacksons and her fourteenth birthday party was at Michael Jackson's infamous Neverland Ranch.

3 ) She lost her virginity young.

"I was young. I had a boyfriend for four years…my first boyfriend. I was with him when I was 14; I’d say around late 14 or early 15, I don’t remember. We were sooo in love; I thought we were going to get married. " Did we just figure out she lost her virginity to a Jackson?

2 ) Kim's godmother is Sugar Ray's wife, Bernadette Leonard.

1) KK sleeps in lingerie every single night, whether she's alone or not.

"I like to wake up feeling good. You’d think a guy was coming over. Sometimes if I’m by myself I’ll wear cottony ones instead of lace ones and my girlfriends or sisters will come over, and they’ll be like, 'Who is coming over? You’re so weird. There’s no guy around; what are you doing?' But it’s totally for me."


Sunday, July 25, 2010

X-PLASTERZ.......!!


In the vibrant Tanzanian hiphop scene, the group X Plastaz is one of the most familiar names, with a huge following especially among the ‘common people’. Their conscious Swahili rap lyrics strike a chord with the Tanzanian youth, who can relate to their topics like Aids, unemployment, divorce and even life in prison. Their music is a unique mixture of traditional chanting and elements from hip hop, ragga and even Hindi music.

Six plastaz
The group consists of six rappers/singers. The three brothers Ruff, Gsann and Ziggy used to work in a haircutting saloon in the heart of Maasai land (northern Tanzania). In recent years they have joined forces with Yamat Ole Meipuko, a Maasai singer who still lives in a traditional Maasai dwelling on a 2 hour's drive from Arusha town. Yamat has won various Maasai singing competitions in his age category, and adds a unique vocal element to the stew of Swahili rhymes and tough hiphop beats. The rappers also tour with their 14 and 16 year old rapping brother and sister who are well known for winning numerous talent awards, defeating even adult rappers. Today, all of them make up the group X Plastaz.

Thursday, July 22, 2010

Muafaka sio kutoa vizuizi walivyoweka wananchi....!!Tunataka matuta!!

Image Askari Polisi wakiondoa vizuizi vilivyowekwa barabarani na wanafunzi katika eneo la Kunduchi Mtongani, Dar es Salaaam, kushinikiza Serikali ijenge matuta barabarani baada ya wanafunzi wawili kugongwa na gari, mmoja alikufa, mwingine amejeruhiwa.(Picha na Robert Okanda).

chonde!!chonde!! jamani tunaelea kwenye uchaguzi mkuu tusifikiwe huku!!


huyu ni moja ya askari wa nchi jirani !!

Nani asiyependa kuishi kwenye mazingira safi!!Tushirikiane kutunza mazingira

Wakazi wa kunduchi mtongani wafunga barabara!!


Mzozo umeibuka baina ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam wanaoishi eneo la Kunduchi Mtongani na askari wa kikosi cha kutuliza ghasia - FFU katika harakati za askari hao kuwaondoa barabarani baada ya wakazi hao kuzuia magari kwa magogo na mawe wakidai barabara hiyo iwekwe matuta. Kutokana na vurugu hizo baadhi ya wakazi hao walijikuta wakikumbana na kipigo kutoka kwa askari hao ambao baada ya kipigo waliwaingiza ndani ya gari la polisi. Hata hivyo baadhi ya wakazi hao walipohojiwa sababu ya azma yao ya kuzuia magari wamesema uamuzi huo umekuja baada ya kugongwa kwa mwanafuzi wa darasa la pili jana ambaye alikufa papo hapo katika eneo hilo.

Monday, July 19, 2010

Hakika wewe ni matata!!


ni moja kati ya wanadada machachari ambao wanapepelusha bendera ya Tanzania ipasavyo katika nyanja za urembo(model) duniani,huyu ni Flavian Matata katika moja pozi pichani

4 SALE

Kuishi ni wajibu ila kuzaa ni majaliwa!

Babu akiwa na mtoto wake

NEW DELHI, India

MZEE mwenye umri wa miaka 90 ameushangaza ulimwengu baada ya kupata mtoto licha ya kuwa na umri huo mkubwa.

Babu huyo, Nanu Ram Jogi ambaye ni mkulima katika kijiji kimoja nchini humo amevunja rekodi yake ya kuzaa katika umri mkubwa ambayo aliishikilia kwa kipindi kirefu cha karne ya 21.

Mwanamume huyo ambaye ameoa mke wa nne katika ndoa zake, anasema hataacha kuzaa mpaka pale atakapotimiza umri wa miaka 100.

Jogi anasema kuwa bado hajapanga idadi kamili ya watoto anaowataka kutoka kwa wake zake hao wanne, lakini anapanga kuwa na watoto wa kiume angalau 12 na wasichana tisa huku akitaraji kuwa na wajukuu 20.


Paka aliyetoweka miezi mitatu arejea
BEDFRORDSHIRE, Uingereza

PAKA aliyewatoroka wenyeji wake miezi mitatu iliyopita amerejea nyumbani alipokuwa akiishi na kuwashangaza watu ambao walidhani kuwa pengine amefariki dunia.

Paka huyo anayejulikana kama alfie anayemilikiwa na Sylivia na Jon Callister alitopoka walipofika katika kituo cha biashara cha Toddington, Bedfordshire Uingereza, wakiwa safarini kurejea Hispania.

"Sikuamini nilipopigiwa simu na idara ya wanyama na kuambiwa kuwa amepatikana akiwa salama," alisema Bw Callister.


Padri aiba sadaka Sh102milioni
NEW HAVEN, Amerika

PADRI mmoja wa Kanisa Katoliki wiki hii aliwashangaza waumini wa kanisa hilo baada ya kuiba sadaka zenye thamani Sh102milioni.

Kiongozi huyo wa kanisa, Kevin J. Gray mwenye umri wa miaka 64 ni kati ya mapadri wanaoaminika, alichukua fedha hizo akiwalaghai waumini wake kwamba ana matatizo ya saratani.

Aliomba ahamishe kiasi cha fedha kwa ajili ya matibabu lakini kinyume na makubaliano ya kanisa, alizitumia kuwaburudisha wanaume pamoja na kuhudhuria matamasha ya watu waliokuwa wakicheza uchi na kununua nguo za bei mbaya.

Alikamatwa katika Hoteli ya Green and Arturo's, New York na kufunguliwa mashtaka yakiwemo ya kumlipia karo ya dola 1.3 milioni mwanamume aliyekutana naye katika bustani ya jiji la New York ili ahudhurie masomo kwenye Chuo cha Havard.


Bibi kizee amjeruhi vibaya mumewe kwa kikaango
MANILA, Ufilipino

MWANAMKE mmoja wa Ufilipino amefikishwa mahakamani baada ya kumjeruhi mumewe kwa kikaango kwa kile kinachodaiwa kuwa ni wivu wa kimapenzi.

Mwanamke huyo mzee wa miaka 50, Kimberly Denocheck alimpiga mumewe mwenye umri wa miaka 48 kwa kikaango hicho, majira ya saa 1: 25 asubuhi wakati alipokuwa akimwandalia kifungua kinywa. Kikaango hicho kilikuwa cha moto kwani ndiyo kwanza kilikuwa kimetoka jikoni.

Mwanamume huyo ambaye amepata majeraha makubwa kichwani, alifikwa na mkasa huo baada ya kuisahau simu yake ya mkononi jikoni hapo alipokuwa akiongea na mkewe na kisha ujumbe mfupi wa maandishi (sms) ukaingia na mkewe huyo kuisoma.

Polisi walisema kuwa mwanamke huyo bado anashikiliwa kituoni huku hali ya mwanamume ikiwa mbaya.

Zimeandaliwa na Herieth Makwetta

Hii ni raha au utamu!??

MWENYEKITI wa Kijiji cha Kemakorere, Zephania Chacha anadaiwa kumshambulia kwa viboko mkuu msaidizi wa Shule ya Sekondari Kemakorere, Juma Selemani Hango akimtuhumu kukata miti miwili ya shule hiyo.

Chacha ameshafikishwa kituo cha polisi kilicho kwenye Kata ya Nyarero wilayani Tarime na anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote kujibu shtaka la kushambulia kwa fimbo na kumsababishia mwalimu huyo maumivu makali.

Tukio hilo ni mwendelezo wa vipigo dhidi ya walimu ambavyo vilianza kusikika baada ya mkuu wa wilaya ya Bukoba, Albert Mnali kuamuru polisi wa kijeshi kuwatandika viboko walimu wa shule tatu kwa madai kuwa ni watoro kazini.

Lakini katika tukio la mkoani Mara, mwenyekiti huyo wa kijiji alichukua hatua hiyo baada ya kupata habari kuwa mkuu huyo msaidizi wa shule alikuwa akikata miti kwenye shamba la shule kwa ajili ya kutengenezea mlango wa choo.

Mkuu wa makosa ya jinai wa Tarime/Rorya, David Hiza alisema kuwa tukio hilo la shambulio hilo dhidi ya Hango lilitokea Julai 5 mwaka huu mchana wakati mwalimu huyo alipokata miti miwili ya shule kwa ajili ya kupasua mbao za kutengenezea mlango wa choo cha shule hiyo.

Hiza alisema kuwa baada ya mwenyekiti huyo kupata taarifa kuwa mwalimu huyo alikuwa akikata miti bila ya ruhusa yake, alienda eneo hilo na kumkuta Mwalimu hango akiendelea na shughuli ya kupasua mbao pamoja na mafundi na ndipo vurugu kubwa ilipozuka.

Alisema katika vurugu hizo, mwenyekiti huyo alichukua fimbo na kuitumia kumshambulia mwalimu huyo na kusababisha apate maumivu sehemu mbalimbali za mwili.

Hiza alisema baadaye mwalimu huyo alifungua jalada namba NY/IR/392/2010 kwenye kituo cha polisi cha Nyamwaga na kwamba mwenyekiti huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote ule.

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kemakorere, Phafin Boroye alisema kuwa uongozi na kamati ya shule hiyo umesikitishwa na kitendo hicho cha mwenyekiti huyo wa kijiji kwa kumshambulia mwalimu wao.

Alisema kuwa miti hiyo ilikuwa kwa ajili ya kupasulia mbao ambazo zingetumika kutengenezea milango ya choo cha shule na kwamba mwalimu huyo hakuwa na nia mbaya kuikata.

Alisema angelipeleka suala hilo kwenye kamati ya shule kama lingekuwa na utata wa ukataji miti hiyo.